Juma Duni Haji achaguliwa Mwenyekiti mpya wa Chama

JUMA DUNI HAJI ACHAGULIWA MWENYEKITI MPYA WA CHAMA TAIFA

Mkutano Mkuu Taifa katika kikao chake kilichofanyika jana tarehe 29 Januari 2022 katika ukumbi wa Mlimani City Dar es salaam, umejaza nafasi za Mwenyekiti wa Chama Taifa, Makamu Mwenyekiti wa Chama Taifa (Zanzibar) na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ambazo zilikuwa wazi kwa sababu mbalimbali.

Kwa upande wa Mwenyekiti wa Chama Taifa, Mkutano Mkuu wa Chama umemchagua Ndugu Juma Duni Haji kujaza nafasi iliyoachwa wazi kufuatia kifo Cha Maalim Seif Sharif Hamad.

Aidha, Mkutano Mkuu umemchagua Ndugu Othman Masoud Othman ambaye pia ni Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar kuwa Makamu Mwenyekiti wa Chama Taifa (Zanzibar).

Kwa upande wa Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama, Mkutano Mkuu Taifa umemchagua Ndugu Msafiri Mtemelwa.

Imetolewa na:

Janeth Joel Rithe,
Naibu Katibu wa Habari, Uenezi na Mahusiano na Umma,
ACT Wazalendo.
30 Januari, 2022.

Showing 1 reaction

Please check your e-mail for a link to activate your account.

Ukurusa huu unatumia kuki. Kusoma zaidi, angalia Vigezo na Masharti yetuOK